@mshambuliaji Avatar @mshambuliaji Maulid Kitenge

Maulid Kitenge posts on X about tanzania, dubai, morocco, leo the most. They currently have [---------] followers and [---] posts still getting attention that total [------] engagements in the last [--] hours.

Engagements: [------] #

Engagements Line Chart

Mentions: [--] #

Mentions Line Chart

Followers: [---------] #

Followers Line Chart

CreatorRank: [-------] #

CreatorRank Line Chart

Social Influence

Social category influence countries 45.18% travel destinations #6716 currencies 4.82% premier league 4.22% finance 3.01% celebrities 2.41% champions league 2.41% social networks 1.81% stocks 1.2% technology brands 1.2%

Social topic influence tanzania #289, dubai 6.02%, morocco #82, leo #912, kwanza 4.82%, caf #72, ethiopia 4.22%, al ahly #8, zanzibar 4.22%, kenya #535

Top accounts mentioned or mentioned by @wasafifm @bintisuleimani @bajabiri @bosskitamb @lordguideshis @mdigala24 @lugumil @tundualissu @officialjux @diamondplatnumz @geraldhando @musakipanya @zembwelabeberu @jokatem @jonmrema @mzeewauvinza @heineken @atikiabdulkarim @abdulsamadtz @jamalmalinzi

Top assets mentioned Uber Technologies, Inc. (UBER) Nani Coin (NANI) TYSON (TYSON)

Top Social Posts

Top posts by engagements in the last [--] hours

"Kikao kilichofanyika jijini Dar es Salaam Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) imethibitisha kuwa michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika [----] haitaahirishwa licha ya kuwepo kwa wasiwasi kuhusiana na maandalizi ya Miundombinu na hali ya hewa ya kisiasa katika nchi waandaaji. Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika Juni-Julai [----] licha ya wito kutoka kwa Mwenyeji mwenza Kenya kufikiria kuahirishwa kutokana na hatari ya vurugu zinazohusishwa na Uchaguzi uliopangwa kufanyika kwa muda huo huo. CAF imesalia kuwa na msimamo imara huku timu ya ukaguzi ikiendelea na kazi"
X Link 2026-02-13T16:37Z 1.8M followers, [----] engagements

"Hili unapaswa kujua ✍🏼"
X Link 2026-02-15T11:18Z 1.8M followers, [----] engagements

"Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete kwa nafasi yake kama Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Elimu Duniani (Global Partnership for Education - GPE) ameshiriki katika Mkutano wa Ngazi ya Juu ulioandaliwa na Taasisi ya Maendeleo ya Umoja wa Afrika (AUDA-NEPAD) Addis Ababa Ethiopia. Mkutano huu uliohusu Mpango wa Sayansi Teknolojia na Uvumbuzi barani Afrika (STISA 2034) ulikutanisha wadau mbalimbali barani Afrika na zaidi kujadili mchango wa Elimu Sayansi Teknolojia na Uvumbuzi katika maendeleo barani Afrika. Rais Mstaafu alisisitiza katika hotuba yake kuwa elimu ni msingi wa maendeleo"
X Link 2026-02-13T16:47Z 1.8M followers, [----] engagements

"Mzee wa Minyama @mshambuliaji amekabidhiwa Tuzo ya kuhamasisha na kufanikisha Kongamano kubwa la Uwekezaji na Biashara la Tanford linalomalizika leo Dubai.✍"
X Link 2026-02-14T13:09Z 1.8M followers, [----] engagements

"Nimefurahishwa na kiwango chenu wote mmeonesha mnaweza msikate tamaa mwakani tutafika. Kauli ya mmiliki wa timu ya Azam FC #yusufbakhresa alipokuwa akiwapa maneno ya faraja wachezaji mara baada ya mchezo dhidi ya Wydad AC hapo jana✍ #KitengeUpdates"
X Link 2026-02-16T04:39Z 1.8M followers, 18.8K engagements

"Mmiliki wa timu ya Azam FC #yusufbakhresa yupo na timu hiyo Casablanca Morocco na leo Jumamosi alipata nafasi ya kula chakula cha mchana pamoja na wachezaji na kuwapa hamasa kuelekea mchezo wa kesho wa hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Wydad AC. #KitengeSports https://twitter.com/i/web/status/2022807619786657993 https://twitter.com/i/web/status/2022807619786657993"
X Link 2026-02-14T22:58Z 1.8M followers, 14.7K engagements

"Klabu ya Simba Sc imeporomoka kutoka nafasi ya tano mpaka nafasi ya [--] kwenye viwango vya ubora wa vilabu barani Afrika ndani ya miaka mitano iliyopita vilivyotoka baada ya kutamatika kwa hatua ya makundi ya michuano ya CAF kwa msimu wa 2025/26. Simba Sc ipo nafasi ya nane ikiwa na pointi [--] huku mahasimu wao Young Africans Sc wakiwa nafasi ya [--] baada ya kukusanya pointi [--] kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Azam FC na Singida Black Stars wapo nafasi ya [--] kila mmoja akiwa na pointi [--]. [--]. Al Ahly - [--] pts [--]. Sundowns - [--] pts [--]. Esperance Tunis - [--] pts [--]. RS Berkane - [--] pts [--]. Pyramids"
X Link 2026-02-16T09:19Z 1.8M followers, 40.8K engagements

"Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) linalaani vikali matukio yasiyokubalika yaliyotokea wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa kati ya Al Ahly ya Misri na ASFAR ya Morocco mjini Cairo Jumapili Februari [--] [----]. CAF imelipeleka suala hilo kwenye Bodi ya Nidhamu kwa uchunguzi na imetaka hatua stahiki zichukuliwe kwa watakaobainika kuhusika baada ya Mashabiki kutupa chupa ndani ya Uwanja na kuzua vurugu. Katika mchezo huo timu zote zilitoka sare ya 0-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya klabu Bingwa Afrika. #KitengeUpdates https://twitter.com/i/web/status/2023394714997678414"
X Link 2026-02-16T13:51Z 1.8M followers, [---] engagements

"Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) linalaani vikali matukio yasiyokubalika yaliyotokea wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa kati ya Al Ahly ya Misri na ASFAR ya Morocco mjini Cairo Jumapili Februari [--] [----]. CAF imelipeleka suala hilo kwenye Bodi ya Nidhamu kwa uchunguzi na imetaka hatua stahiki zichukuliwe kwa watakaobainika kuhusika baada ya Mashabiki kutupa chupa ndani ya Uwanja na kuzua vurugu. Katika mchezo huo timu zote zilitoka sare ya 0-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya klabu Bingwa Afrika. #KitengeUpdates https://twitter.com/i/web/status/2023397042354085971"
X Link 2026-02-16T14:00Z 1.8M followers, [----] engagements

"Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) linalaani vikali matukio yasiyokubalika yaliyotokea wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa kati ya Al Ahly ya Misri na ASFAR ya Morocco mjini Cairo Jumapili Februari [--] [----]. CAF imelipeleka suala hilo kwenye Bodi ya Nidhamu kwa uchunguzi na imetaka hatua stahiki zichukuliwe kwa watakaobainika kuhusika baada ya Mashabiki kutupa chupa ndani ya Uwanja na kuzua vurugu. Katika mchezo huo timu zote zilitoka sare ya 0-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya klabu Bingwa Afrika. #KitengeUpdates https://twitter.com/i/web/status/2023397076889989434"
X Link 2026-02-16T14:00Z 1.8M followers, [----] engagements

"BREAKING: Rasmi kampuni ya GSM Tanzania Limited imeshinda tenda ya kujenga Uwanja wa klabu ya Yanga kwa kushirikiana na klabu hiyo. Rais wa klabu ya Yanga Sc Eng. Hersi Said ndiye Mwenyekiti wa Kamati Maalum iliyoundwa kusimamia ujenzi wa uwanja huo huku Wajumbe wa kamati hiyo watakuwa ni Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji ya Yanga SC. Kamati hiyo itakutana na GSM Tanzania Limited kujadili kuanza kwa mradi huo. #KitengeSports https://twitter.com/i/web/status/2018258802873696674 https://twitter.com/i/web/status/2018258802873696674"
X Link 2026-02-02T09:42Z 1.8M followers, 60.5K engagements

"Aliyewahi kuwa Mbunge Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Munde Tambwe amefariki Dunia baada ya kuugua kwa kipindi sasa. Katika uhai wake Marehemu Munde alikuwa Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Tabora. #KitengeUpdates"
X Link 2026-02-03T03:56Z 1.8M followers, 16.3K engagements

"Kupitia tovuti zao Ubalozi wa Marekani umetangaza kufunga Balozi zao nchini Burundi Rwanda na Uganda. Hii ilitokana na ukosefu wa Fedha katika Balozi hizo baada ya Marekani kuchukua hatua kadhaa kukomesha matumizi ya Marekani nje ya nchi. Hatua hiyo imekuja baada ya hivi karibuni Marekani kusitisha VISA kwa nchi nyingi ikiwemo Burundi na nchi mbali mbali barani Afrika. Sio tu huko ambako Balozi zimefungwa kwa sababu zimefungwa pia katika nchi nyingine mfano Ethiopia na nchi nyingine nyingi. Itakumbukwa kuwa Mabalozi wa Marekani katika nchi hizo waliitwa hivi karibuni Washington DC kwa agizo"
X Link 2026-02-03T15:52Z 1.8M followers, 61.9K engagements

"Kampuni ya Uber ambayo hutoa huduma ya usafiri ya teksi kwa njia ya mtandao kwa mara nyingine imetangaza kusitisha shughuli zake nchini Tanzania kuanzia Januari [--] [----] kutokana na changamoto za kibiashara. Mara ya kwanza kampuni hiyo ilisitisha utoaji wa huduma Aprili [----] hadi Januari [----] kwa sababu kama hizo. Leo Jumanne Februari [--] [----] akizungumza Ofisa Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mahusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (Latra) Salum Pazzy amesema taarifa zilizokuwa zikisambaa kuwa Uber imejiondoa nchini ni sahihi na wamepokea barua rasmi. Ni kweli kumekuwa na taarifa"
X Link 2026-02-03T17:27Z 1.8M followers, 11.3K engagements

"Rais wa Marekani Donald Trump amesema hawezi kuomba radhi kwa kufuatia kusambaa kwa video iliyopostiwa katika ukurasa wake wa Truth Social ikiwaonesha Rais mstaafu Barack Obama na mkewe Michelle Obama katika sura ya Nyani. Trump amedai kuwa video ile aliiona mwanzoni tu hakuiona sehemu hiyo ya video kabla ya kuiposti na lengo lake lilikuwa ni kuonesha ujumbe kuhusu udanganyifu wa kura wa mwaka [----] uliokuwemo mwanzoni mwa video hiyo. Trump ameongeza kuwa video hiyo ilikuwa ni vichekesho vya mtandaoni vilivyochukuliwa kutoka kwenye filamu ya The Lion King ambapo viongozi wengi wa kisiasa"
X Link 2026-02-07T11:34Z 1.8M followers, 11.1K engagements

"Mfanyabiashara Said Hamad Lugumi (@LugumiL ) amesherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kula na Watoto Yatima [---] huku akisema miaka [--] akijivunia kuwa hamfitini Mtu Simdhulumu Mtu wala sifanyi Majungu. Ameyasema hayo leo wakati alipoandaa Chakula maalum kusherehekea siku yake ya kuzaliwa Nyumbani kwake. #KitengeUpdates"
X Link 2026-02-07T13:53Z 1.8M followers, 23.1K engagements

"Idara ya sheria ya Marekani imemfungulia mashtaka Shannon Mathre wa Ohio kwa kutishia kumuua Makamu wa Rais wa Marekani J.D. Vance. Mshukiwa huyo mkazi wa Toledo Ohio alikamatwa na maafisa wa U.S Secret Service Februari [--] [----] kwa madai ya kutishia kumuua na kumjeruhi Makamu wa Rais wa Marekani. Mbali na shtaka la kumtishia Vance waendesha Mashtaka pia walimshtaki Shannon Mathre kwa kumiliki faili za kidijitali zinazoonyesha unyanyasaji wa kingono kwa watoto ambazo ziligunduliwa wakati wa uchunguzi. Shtaka hilo la pili linaweza kuwa na adhabu kali zaidi ya hadi miaka [--] jela. Shtaka"
X Link 2026-02-08T14:55Z 1.8M followers, [----] engagements

"Wawakilishi wa Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC) wamesukumizwa nje ya michuano hiyo kufuatia kipigo cha 1-0 dhidi ya Sead Ramovic na vijana wake wa CR Belouizdad katika dimba la New Amaan Complex Zanzibar kwenye mchezo wa kundi C wa CAFCC. : - ⚽ 03' Belhocini [--]. - [--] [--]. ' - [--] [--]. - [--] [--]. - [--] MECHI ZA MWISHO KUNDI C CAFCC CR Belouizdad Otoho d'Oyo Stellenbosch Singida Black Stars #KitengeSports"
X Link 2026-02-08T18:31Z 1.8M followers, 11K engagements

"Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Zimbabwe Mhe. CP Suzan Kaganda amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi pamoja na Wanachama wa Jumuiya za Watanzania wanaoishi katika maeneo ya Hwange na Bulawayo nchini Zimbabwe. Lengo la Mkutano huo lilikuwa ni kujadili masuala mbalimbali yanayowahusu Watanzania wanaoishi nje ya nchi yakiwemo ushiriki wao katika utekelezaji wa sera ya Diplomasia ya Uchumi pamoja na sera ya lugha ya Kiswahili. Katika mazungumzo hayo Balozi CP Kaganda ametoa wito kwa Watanzania wanaoishi ughaibuni kuhakikisha wanajisajili katika mfumo wa Diaspora Hub"
X Link 2026-02-10T04:27Z 1.8M followers, [----] engagements

"Waziri wa habari wa Uganda Chris Baryomunsi amelaani uvamizi wa Kijeshi wa mwezi uliopita katika Nyumba ya Kiongozi wa upinzani Bobi Wine kwamba Wine hakufanya uhalifu wowote na ana haki ya kurejea Nyumbani. Wine Mwanamuziki wa Pop aliyegeuka Mwanasiasa ambaye jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi amekuwa mafichoni kwa wiki kadhaa baada ya kutoroka Nyumbani kwake katika Mji Mkuu Kampala saa chache baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa pili katika uchaguzi wa Urais. Rais Yoweri Museveni ambaye amekuwa madarakani kwa miaka [--] alitangazwa mshindi wa uchaguzi huo. Mnamo Januari [--] Wine aliripoti"
X Link 2026-02-10T11:47Z 1.8M followers, 12.6K engagements

"Joan Laporta amejiuzulu kama Rais wa FC Barcelona akinuia kugombea tena katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Machi [--]. Kanuni za klabu zinaelekeza kuwa Rais wa sasa anatakiwa kuachia ngazi kabla ya uchaguzi huku kamati ya usimamizi ikihakikisha mwendelezo wa shughuli za klabu katika kipindi hiki. Kamati hii itaongozwa na Rafa Yuste Makamu wa Rais wa Laporta tangu kuchaguliwa kwake [----]. Laporta atachuana na wagombea wanne wa kiti cha Urais Vctor Font Marc Ciria Xavier Vilajoana na Joan Camprub ambao wote wametangaza nia zao. Ili kujitokeza kwenye kura mnamo Machi [--] lazima wakusanye sahihi"
X Link 2026-02-10T17:02Z 1.8M followers, 15.9K engagements

"Wafanyakazi wa Ndege nchini Kenya wanapanga kugoma wiki ijayo na hivyo kutatiza shughuli katika Viwanja vya Ndege nchini humo kulingana na barua kutoka kwa chama chao kwa Mamlaka. Katika barua iliyotumwa kwa Mamlaka ya usafiri wa Anga ya Kenya (KCAA) mnamo Februari [--] Muungano wa Wafanyakazi wa usafiri wa Anga nchini Kenya ulitoa notisi ya muda siku saba kabla ya kugoma. Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta wa Nairobi ni mojawapo ya Viwanja vya Ndege vilivyo na shughuli nyingi zaidi Afrika Mashariki na katika bara la Afrika. Bado haijajulikana ni Wafanyakazi wangapi wanaweza kugoma."
X Link 2026-02-10T17:05Z 1.8M followers, [----] engagements

"Mahakama Kuu ya Zambia Kitengo cha makosa ya rushwa na Uhujumu Uchumi imetaifisha mali za Dalitso Lungu Mtoto wa kiume wa aliyekuwa Rais wa zamani wa nchi hiyo Edgar Lungu. Hukumu hiyo imesomwa leo mjini Lusaka ambapo mali zilizotaifishwa ni Magari [--] yakiwemo Magari ya Kifahari kama Rolls Royce Mercedes-Benz Ferrari na Lamborghini ambayo amekuwa akionekana nayo katika maeneo ya Kifahari mjini Lusaka na Afrika Kusini. Pamoja na magari hayo pia Mahakama imetaifisha kituo kimoja cha Mafuta Mjini Lusaka kilichokuwa kinamilikiwa na Dalitso pamoja na nyumba [--] za Kifahari alizonunua maeneo ya Ibex"
X Link 2026-02-10T17:35Z 1.8M followers, 13.7K engagements

"Bao pekee la Joao Pedro linaipeleka Chelsea mapumzikoni vifua mbele dhidi ya Leeds United katika dimba la Stamford Bridge. HT: Chelsea 1-0 Leads United ⚽ 24' Joao Pedro HT: Everton 1-0 Bournemouth HT: Tottenham 0-1 Newcastle United #KitengeSports"
X Link 2026-02-10T20:33Z 1.8M followers, [----] engagements

"Chelsea imelazimishwa sare ya 2-2 ikiwa nyumbani dhidi ya Leeds United katika dimba la Stamford Bridge baada ya kuongoza 2-0 kwa takribani dakika [--]. FT: Chelsea 2-2 Leeds United ⚽ 24' Pedro ⚽ 58' Palmer ⚽ 67' Nmecha (P) ⚽ 73' Okafor FT: Tottenham 1-2 Newcastle United FT: Everton 1-2 Bournemouth FT: West Ham United 1-1 Man United #KitengeSports https://twitter.com/i/web/status/2021349482550403094 https://twitter.com/i/web/status/2021349482550403094"
X Link 2026-02-10T22:24Z 1.8M followers, [----] engagements

"Klabu ya Tottenham Hotspur imethibitisha kumfuta kazi kocha Thomas Frank kama Kocha mkuu klabuni hapo kufuatia mfulululizo wa matokeo yasiyoridhisha ikiwemo kichapo cha 2-1 dhidi ya Newcastle United siku ya Jumanne. Frank (51) raia wa Denmark aliteuliwa kuwa Kocha mkuu wa klabu hiyo mnamo Juni [----] akitokea Brentford na kuchukua mikoba ya Ange Postecoglou. Spurs sasa ipo sokoni kusaka kocha mwingine ambaye atakuwa kocha wa tano kuinoa timu hiyo tangu [----] huku Mauricio Pochettino Oliver Glasner Xabi Alonso na Marco Silva wakitajwa kuwa mstari mbele kuchukua mikoba ya Thomas Frank."
X Link 2026-02-11T11:44Z 1.8M followers, [----] engagements

"James Van Der Beek Muigizaji maarufu aliyepata umaarufu kwa kuigiza kwenye tamthilia ya vijana ya miaka ya [----] Dawsons Creek amefariki dunia akiwa na umri wa miaka [--]. Familia yake ilitangaza kupitia ukurasa wake wa Instagram kwamba alifariki kwa amani asubuhi ya tarehe [--] Februari [----] kwa maradhi ya saratani ya utumbo mpana (colorectal cancer) ambayo alikuwa akipigania tangu [----]. Familia ilisema aliishi siku zake za mwisho kwa ushujaa imani na neema na sasa wanaomba faragha wakati wa kuomboleza. Van Der Beek alitangaza kuwa anaishi na stage [--] colorectal cancer (saratani ya utumbo mpana)"
X Link 2026-02-11T21:00Z 1.8M followers, [----] engagements

"Manchester City imeibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Fulham katika dimba la Etihad na kusogea mpaka alama tatu nyuma ya Arsenal ambao Wana mchezo mmoja mkononi. Man City imefikisha alama [--] baada ya mechi [--] huku ikiendelea kusalia nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi kuu England. FT: Man City 3-0 Fulham ⚽ 24' Semenyo ⚽ 30' O'Reilly ( Semenyo) ⚽ 38' Haaland ( Foden) FT: Aston Villa 1-0 Brighton FT: Crystal Palace 2-3 Burnley FT: Nottingham Forest 0-0 Wolves #KitengeSports https://twitter.com/i/web/status/2021702543295098947 https://twitter.com/i/web/status/2021702543295098947"
X Link 2026-02-11T21:47Z 1.8M followers, [----] engagements

"Binti Anastazia Daudi Masaniro ambaye ni mhitimu wa Chuo Kikuu Dar es salaam anaomba Msaada wa haraka wa matibabu baada ya kupata ajali mbaya ya pikipiki iliyopelekea mguu wake kujeruhiwa vibaya na sasa una maambukizi hatari. Anastazia anahitaji upasuaji wa haraka ili kuzuia maambukizi na kuokoa maisha yake. Mchango wako hata kama ni mdogo unaweza kuleta tofauti kubwa. Kiasi kinachohitajika: TZS [-------] Tuma mchango wako kupitia: M-PESA +255 [---] [---] [---] ANASTAZIA DAUDI MASANIRO #KitengeUpdates"
X Link 2026-02-11T22:20Z 1.8M followers, 38.4K engagements

"Liverpool imeibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Sunderland katika dimba la Stadium of Light na kukomesha rekodi ya Paka hao Weusi ya kutopoteza nyumbani (unbeaten) tangu msimu huu uanze. FT: Sunderland 0-1 Liverpool ⚽ 61' van Dijk #KitengeSports"
X Link 2026-02-11T22:30Z 1.8M followers, [----] engagements

"RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini leo tarehe [--] Februari [----] kuelekea Addis Ababa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Shirikisho la Ethiopia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa [--] wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) utakaofanyika tarehe [--] hadi [--] Februari [----]. Taarifa ya leo Januari [--] [----] iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu Bakari S. Machumu imeeleza kuwa kabla ya kuanza kwa Mkutano Mkuu tarehe [--] Februari [----] Rais Samia anatarajiwa kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi"
X Link 2026-02-12T09:14Z 1.8M followers, [----] engagements

"Wananchi wakilia kwa uchungu Mahakama Kuu baada ya Mhe. Tundu Lissu kutokula mchana wa leo baada ya mapumziko ya muda mfupi. Wananchi wengine walizimia. Lissu Mwenyekiti wa Chadema anayekabiliwa na kesi ya Uhaini alilalamika leo kutopewa Chakula. #KitengeUpdates"
X Link 2026-02-12T13:51Z 1.8M followers, 15K engagements

"Ka Chai ka Dubai☕"
X Link 2026-02-12T14:28Z 1.8M followers, [----] engagements

"Maafisa wa usalama wa Rais wa Kenya William Ruto wamelazimika kuingilia kati kuzuia kijana mmoja aliyetaka kulisogelea jukwaa wakati Rais akiwahutubia washiriki wa kongamano la kibiashara la NYOTA Business Forum. Tukio hilo limetokea wakati wa hafla ya kutoa mitaji kwa wafanyabiashara wapya (start-ups) ambapo maafisa walimnasa mwanamume huyo kwa haraka kabla ya kufika jukwaani na kumdhibiti. Baada ya hali ya utulivu kurejea Rais Ruto alitoa maelekezo kwa timu yake ya ulinzi kumshikilia mwanamume huyo kwa muda akiahidi kushughulikia jambo lake baadaye. #KitengeUpdates"
X Link 2026-02-12T16:36Z 1.8M followers, 15.9K engagements

"Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amemchagua Binti yake Kim Ju Ae kurithi nafasi yake ya Urais. Uthibitisho huo unakuja baada Binti huyo kuonekana mara kwa mara kwenye hafla za Serikali mara nyingi akiandamana na Baba yake katika hafla zinazoonekana kuwa za kisiasa. Kim Ju Ae anayeaminika kuwa na umri wa miaka [--] alionekana hadharani kwa mara ya mwisho mnamo [----] alipoandamana na babake kukagua kombora la masafa marefu. Tangu wakati huo ameonekana mara kwa mara kwenye vyombo vya habari vya serikali kwenye gwaride la kijeshi na ziara za serikali pamoja na safari ya hivi karibuni ya"
X Link 2026-02-12T17:14Z 1.8M followers, 17.4K engagements

"Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa onyo rasmi na kupiga marufuku matumizi ya noti za shilingi za Kitanzania (TZS) kutengeneza mashada ya maua (cash bouquets) mapambo au garlands za maua na vitu vingine vya sherehe kuelekea msimu wa Valentine Gavana wa benki hiyo Emmanuel Tutuba amesema kitendo hicho ni uharibifu wa fedha za taifa (defacement of currency) na ni kinyume cha sheria na kubainisha kwamba watakaobainika kutenda kosa hilo wanaweza kukabiliwa na adhabu ya faini ya hadi Shilingi Milioni tano. Sababu ya marufuku hiyo ni kwamba kukunja kubandika kushona au kuweka noti hivyo huharibu"
X Link 2026-02-12T21:16Z 1.8M followers, [----] engagements

"Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika [----] itakayofanyika Kenya Uganda na Tanzania inaweza kuahirishwa kutokana na Maandalizi kusua sua. Kamati ya utendaji ya Shirikisho la soka Afrika (CAF) inatarajiwa kukutana jijini Dar es Salaam Tanzania Ijumaa ya leo Februari [--] [----]. Inaelezwa kuwa tayari Tanzania na Uganda zimelipa Dola Milioni [--] kuandaa michuano hiyo lakini Kenya bado haijalipa haki kamili. Ikiwa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika itaahirishwa itasogezwa hadi [----] kwani kuanzia hapo michuano hiyo itachezwa kila baada ya miaka minne badala ya kila baada ya miaka miwili. Kikao cha"
X Link 2026-02-13T06:19Z 1.8M followers, 22.4K engagements

"Nyota wa Italia Mtukutu Super Mario Balotelli amesema amefanyiwa vitendo vya ubaguzi wakati wa mechi ya Ligi daraja la pili katika Falme za Kiarabu kati ya Dubai na Al-Ettifaq. Katika taarifa iliyochapishwa kwenye akaunti yake ya Instagram Mshambuliaji huyo wa Kiitaliano ambaye zamani alikuwa akiichezea Marseille alifichua kwamba alivumilia unyanyasaji wa mara kwa mara ambao amekuwa akikukatana nao. Leo wakati wa mechi nilifanyiwa vitendo vya kibaguzi mara kadhaa. Niliambiwa mara kwa mara nenda kula ndizi Balotelli aliandika. Alikemea vikali tabia hiyo akisisitiza hakuna nafasi ya ubaguzi wa"
X Link 2026-02-13T07:13Z 1.8M followers, 16.1K engagements

"Wenyeji wenza wa Mashindano ya AFCON [----] Kenya wameunga mkono hoja ya kutaka kuahirishwa kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) [----] kutokana na uwezekano wa vurugu zinazohusiana na uchaguzi wa Kenya katika kipindi hicho. Ripoti katika gazeti la Uingereza The Guardian Jumatano ilisema kuwa mashindano hayo yanaweza kuahirishwa hadi [----] kwa sababu Kenya Uganda na Tanzania bado hawako tayari kuandaa Mashindano hayo. Timu ya ukaguzi kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwa sasa iko Tanzania na inafanya mkutano leo kuhusu maandalizi. Rais wa CAF Patrice Motshepe hapo awali amesema kuwa ana"
X Link 2026-02-13T09:19Z 1.8M followers, 15.3K engagements

"Meneja wa Manchester United Michael Carrick amechaguliwa kuwa Kocha bora wa mwezi Januari wa Ligi kuu England akitwaa tuzo hiyo kwenye mwezi wake wa kwanza tu tangu ateuliwe kuwa Kocha wa klabu hiyo. Carrick [--] raia wa England anakuwa kocha wa pili wa Manchester United kutwaa tuzo hiyo baada ya mtangulizi wake Ruben Amorim aliyetwaa tuzo hiyo mwezi Oktoba [----]. WASHINDI WA TUZO YA KOCHA BORA WA MWEZI EPL 2025/26 Agosti: Arne Slot (Liverpool) Septemba: Oliver Glasner (Crystal Palace) Oktoba: Ruben Amorim (Man Utd) Novemba: Enzo Maresca (Chelsea) Desemba: Unai Emery (Aston Villa) Januari:"
X Link 2026-02-13T16:33Z 1.8M followers, [----] engagements

"Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) inaendelea tena leo Februari [--] [----] kwa mechi sita za kuhitimisha hatua ya makundi kwa msimu wa 2025/26 huku wawakilishi wa Tanzania kwenye CAFCL Simba Sc wakikamilisha ratiba baada ya kuondoshwa. Simba Sc ambayo imeshindwa kufuzu ikishindwa kupata ushindi wowote kwenye mechi tano (vipigo vitatu sare mbili) itakuwa nyumbani Benjamin Mkapa kuvaana na Stade Malien ya Mali majira ya saa 1:00 usiku ikiwa ni mchezo wa kundi D wa CAFCL. Kwenye mchezo mwingine wa kundi hilo Esperance de Tunis ya Tunisia watakuwa wenyeji wa Petro De Luanda ya Angola huku"
X Link 2026-02-14T10:37Z 1.8M followers, [----] engagements

"imemtambulisha beki wa zamani wa Simba Sc na timu ya Taifa ya Tanzania Erasto Edward Nyoni ambaye anamudu kucheza kama kiungo kama mchezaji mpya klabuni hapo Nyoni ambaye pia amewahi kuvichezea vilabu vya Vital'O FC ya Burundi Azam FC na Namungo FC anatua kwa Wanankurukumbi akitokea Klabu ya New King inayoshiriki Ligi kuu Zanzibar #KitengeSports https://twitter.com/i/web/status/2022632820405871012 https://twitter.com/i/web/status/2022632820405871012"
X Link 2026-02-14T11:23Z 1.8M followers, 22.2K engagements

"Mtangazaji wa Michezo wa @wasafifm Mwanaid Suleiman (@bintisuleimani) akiwa katika usiku wake na Mume wake Brigedia Jenerali Hassan Rashid Mabena baada ya kufunga ndoa yao. #KitengeUpdates"
X Link 2026-02-14T19:16Z 1.8M followers, 34.4K engagements

"Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda akiwa kwenye usiku wa Mtangazaji wa @wasafifm Mwanaid Suleiman (@bintisuleimani ) na Brigedia Jenerali Hassan Rashid Mabena ambao wamefunga ndoa Jijini Dar es Salaam. #KitengeUpdates"
X Link 2026-02-14T21:49Z 1.8M followers, 15.2K engagements

"@bajabiri Hana mpinzani"
X Link 2026-02-15T14:31Z 1.8M followers, [----] engagements

"Makocha [---] wametuma maombi ya kuifundisha timu ya Taifa ya Rwanda Amavubi ambayo imekaa mwezi mmoja bila Kocha Mkuu. Shirikisho la soka la Rwanda (FERWAFA) liliachana na aliyekuwa Kocha wa timu hiyo Adel Amrouche Januari [--] [----] baada ya kuhudumu kwa mwaka mmoja. Wakati mchakato wa kutafuta mbadala wake ukiendelea FERWAFA ilitangaza kupokea maombi ya Makocha [---] wenye sifa ambayo yatafuatiwa na hatua ya mchujo kwa kuzingatia sifa na uzoefu wa kufundisha timu za taifa na ushiriki wao katika michuano mikubwa ikiwemo Kombe la Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia. Rwanda itaandaa mechi za"
X Link 2026-02-14T11:57Z 1.8M followers, [----] engagements

"Rais wa Makampuni ya GSM Mfadhili na mdhamini wa Klabu ya Yanga Ghalib Said Mohamed katika mkutano wa majadiliano kati ya Kamati Maalum ya Ujenzi wa Uwanja wa Yanga na Mwekezaji unaofanyika Zanzibar. #KitengeSports"
X Link 2026-02-14T12:56Z 1.8M followers, [----] engagements

"Mnyama Simba Sc anaelekea mapumzikoni vifua mbele dhidi ya Stade Malien ya Mali katika dimba la Benjamin Mkapa kwenye mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) HT: Simba Sc 1-0 Stade Malien ⚽ 03' Oura #KitengeSports"
X Link 2026-02-14T16:56Z 1.8M followers, [----] engagements

"Wekundu wa Msimbazi Simba Sc wamepata ushindi wa kwanza kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya vinara wa kundi D Stade Malien katika dimba la Benjamin Mkapa. Kwenye mchezo mwingine wa kundi hilo Esperance de Tunis imeilaza Petro De Luanda mabao 2-0 na kuungana na Stade Malien kwenye hatua ya robo fainali huku Simba Sc na Petro Luanda kuaga mashindano hayo. FT: Simba Sc 1-0 Stade Malien ⚽ [--] Anicet Oura Esperance Tunis 2-0 Petro De Luanda ⚽ [--] Diakite ⚽ [--] Diarra MSIMAMO KUNDI D [--]. Stade Malien - pointi [--] (+3) [--]. Esperance - pointi [--] (+2)"
X Link 2026-02-14T18:12Z 1.8M followers, [----] engagements

"Wakati Wafanyabiashara wa nchi zingine wakiutumia Mwezi wa Ramadhan kupandisha bidhaa Wenzao wa Falme za Kiarabu wao wanautumia Mwezi wa Ramadhan kuitafuta Pepo kwa kushusha maradufu bei za Bidhaa. #KitengeUpdates"
X Link 2026-02-14T20:59Z 1.8M followers, 10.8K engagements

"Timu ya Waendesha Baiskeli ya Cycling Brothers toka Tanzania imefanya vizuri katika Spinneys Dubai [--] Cycle Challenge ambayo ni Mashindano ya Baiskeli maarufu yanayofanyika kila mwaka huko Dubai Falme za Kiarabu (UAE) yaliyofanyika hii leo na kufanikiwa kufuzu kwa Mashindano makubwa ya UCI Gran Fondo World Championships huko Niseko Japan mwezi wa Agosti Mwaka huu. #KitengeUpdates https://twitter.com/i/web/status/2023042473224786057 https://twitter.com/i/web/status/2023042473224786057"
X Link 2026-02-15T14:31Z 1.8M followers, [----] engagements

"Wanalambalamba Azam FC wamesukumizwa nje ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCL) kufuatia kipigo cha 2-0 ugenini dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco kwenye mchezo wa mwisho wa kundi B. Kwenye mchezo mwingine wa kundi hilo Nairobi United imekamilisha ratiba kwa kipigo cha 3-0 dhidi ya Maniema ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. FT: Wydad AC 2-0 Azam FC ⚽ 64' Msindo (og) ⚽ 90+4' Nassi FT: Maniema 3-0 Nairobi United ⚽ 05' Namboka ⚽ 29' Namboka ⚽ 44' Mboma Kinda 🟥 57' Machaga MSIMAMO KUNDI B [--]. Wydad AC - pointi [--] [--]. Maniema - pointi [--] [--]. Azam FC - pointi [--] [--]. Nairobi Utd - pointi"
X Link 2026-02-15T16:27Z 1.8M followers, [----] engagements

"Wananchi Young Africans Sc wanaelelea mapumzikoni vifua mbele dhidi ya vigogo wa Algeria JS Kabylie katika dimba la New Amaan Complex Zanzibar huku Al Ahly na AS FAR Rabat wakitoshana kwa sare tasa katika dimba la Cairo International. HT: Yanga Sc 1-0 JS Kabylie ⚽ 38' Depu HT: Al Ahly 0-0 FAR Rabat #KitengeSports https://twitter.com/i/web/status/2023084682024243597 https://twitter.com/i/web/status/2023084682024243597"
X Link 2026-02-15T17:19Z 1.8M followers, [----] engagements

"Shughuli ya imemalizika katika dimba la New Amaan Complex Zanzibar huku wananchi Young Africans Sc wakisukumizwa nje ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) baada ya Al Ahly kutoshana nguvu na AS Far Rabat kwa sare tasa licha ya Yanga Sc kushinda kwa kishindo. AS Far Rabat wameungana na Al Ahly kwenye robo fainali ya michuano hiyo huku Yanga Sc ikiungana na Simba Sc Azam FC na Singida Black Stars kurudi nyumbani baada ya timu zote kutoka Tanzania kuaga michuano ya CAF msimu huu. FT: Yanga Sc 3-0 JS Kabylie ⚽ [--] Depu ⚽ [--] Depu ⚽ [--] Boka FT: Al Ahly 0-0 FAR Rabat MSIMAMO KUNDI B kwenye mabano"
X Link 2026-02-15T18:16Z 1.8M followers, 11K engagements

"Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Shirikisho ya Somalia wamesaini Hati ya Makubaliano kuhusu masuala ya kiuhamiaji. Hati hiyo ya Makubaliano imelenga kuondoleana hitaji la visa kwa Pasipoti za kidiplomasia na za kiutumishi pamoja na mashirikiano katika masuala ya uhamiaji baina ya nchi hizo mbili. Hati hiyo ya Makubaliano imesainiwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Patrobas Katambi na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Serikali ya SomaliaJenerali Abdullahi Sheikh Ismail Fartaag. Akizungumza baada ya kusaini Hati ya Makubaliano"
X Link 2026-02-16T15:45Z 1.8M followers, [----] engagements

"Laurindo Dilson Maria Aurlio 'Depu' anaiandikia Young Africans Sc bao la uongozi kwa mkwaju wa penalti dhidi ya JS Kabylie ya Algeria katika dimba la New Amaan Complex Zanzibar. Yanga Sc 1-0 JS Kabylie ⚽ 35' Depu #KitengeSports"
X Link 2026-02-15T16:43Z 1.8M followers, [----] engagements

"Kocha Miguel Angel Gamondi amesaini mkataba wa kudumu wa miaka miwili wa kuinoa Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' baada ya kuonesha uwezo mkubwa kwa kipindi kifupi alichohudumu kama kocha wa muda akiiongoza Stars kufuzu hatua ya [--] bora ya AFCON [----] kwa mara ya kwanza kihistoria. Hafla ya Utiaji Saini Mkataba wa Kocha huyo raia wa Argentina imefanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa ambapo sasa kocha huyo wa zamani wa Yanga Sc atakuwa na jukumu la kuiongoza Stars kwenye michuano AFCON [----] ambapo Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano hayo. #KitengeSports"
X Link 2026-02-16T08:39Z 1.8M followers, [----] engagements

"Ndege ya Shirika la Ndege la Kenya iliyopangwa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kigali ilirejea Nairobi baada ya kukumbwa na hali mbaya ya hewa. Ndege hiyo ilijaribu kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kigali mara mbili lakini hali ya hewa ilikuwa mbaya jambo lililomzuia Rubani kuona njia ya kurukia Ndege vizuri. Shirika la ndege la Kenya Airways lilisema kuwa baada ya majaribio mawili bila mafanikio Wafanyakazi wa Ndege hiyo waliamua kurejea Nairobi kwa usalama wa abiria na Wafanyakazi. Tukio hilo limesababisha kuchelewa kwa safari za Ndege nyingine ikiwa ni pamoja na"
X Link 2026-02-16T12:57Z 1.8M followers, [----] engagements

"Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) linalaani vikali matukio yasiyokubalika yaliyotokea wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa kati ya Al Ahly ya Misri na ASFAR ya Morocco mjini Cairo Jumapili Februari [--] [----]. CAF imelipeleka suala hilo kwenye Bodi ya Nidhamu kwa uchunguzi na imetaka hatua stahiki zichukuliwe kwa watakaobainika kuhusika baada ya Mashabiki kutupa chupa ndani ya Uwanja na kuzua vurugu. Katika mchezo huo timu zote zilitoka sare ya 0-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya klabu Bingwa Afrika. #KitengeUpdates https://twitter.com/i/web/status/2023394478476722401"
X Link 2026-02-16T13:50Z 1.8M followers, 28.3K engagements

"Shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) linalaani vikali matukio yasiyokubalika yaliyotokea wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa kati ya Al Ahly ya Misri na ASFAR ya Morocco mjini Cairo Jumapili Februari [--] [----]. CAF imelipeleka suala hilo kwenye Bodi ya Nidhamu kwa uchunguzi na imetaka hatua stahiki zichukuliwe kwa watakaobainika kuhusika baada ya Mashabiki kutupa chupa ndani ya Uwanja na kuzua vurugu. Katika mchezo huo timu zote zilitoka sare ya 0-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya klabu Bingwa Afrika. #KitengeUpdates https://twitter.com/i/web/status/2023395100248719678"
X Link 2026-02-16T13:52Z 1.8M followers, [----] engagements

"Safari za Ndege kuingia na kutoka katika Uwanja Mkuu wa Ndege wa Kenya zimecheleweshwa kufuatia mgomo uliopangwa wa Wafanyakazi wa sekta ya anga. Safari za Ndege zinazoondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi mojawapo ya viwanja vya usafiri vilivyo na shughuli nyingi zaidi barani Afrika zimecheleweshwa kwa hadi saa nne. Baadhi ya abiria wanasema wamekaa ndani ya Ndege kwa muda mrefu huku Marubani wakisubiri kibali kupaa. Katika taarifa Shirika la Ndege la Kenya Airways lilisema linakabiliwa na kucheleweshwa kwa uendeshaji wa udhibiti wa trafiki ya anga na"
X Link 2026-02-17T10:06Z 1.8M followers, [----] engagements

"Mchungaji Jesse Jackson ambaye ni mfuasi wa Martin Luther King Jr ambaye aliongoza harakati za haki za kiraia kwa miongo kadhaa baada ya kuuawa kwa Luther amefariki dunia leo Jumanne akiwa na umri wa miaka [--] akiwa amezungukwa na familia yake. Jackson ambaye alikuwa Mgombea urais mara mbili nchini Marekani chini ya Chama cha Democratic mwaka [----] na [----] aliitwa kukutana na King katika Hoteli ya Lorraine jijini Memphis muda mfupi kabla hajauawa kwa kupigwa risasi na baadaye alijiweka hadharani kama mrithi wa King. Jackson aliongoza maisha ya mapambano nchini Marekani na Kimataifa akitetea"
X Link 2026-02-17T12:59Z 1.8M followers, [----] engagements

"Natembea na chakula Mhe. @TunduALissu leo Mahakamani✍"
X Link 2026-02-17T14:11Z 1.8M followers, 11.3K engagements

"Hili muhimu sana kufahamu✍🏼"
X Link 2026-02-13T09:33Z 1.8M followers, [----] engagements

"Huyu pia ni Adui yako ✍🏼"
X Link 2026-02-13T15:24Z 1.8M followers, [----] engagements

"Magwiji wa Ndondi Mike Tyson na Floyd Mayweather wanatazamiwa kupigana katika pambano la maonyesho nchini DR Congo Aprili [-----]. Tyson na Mayweather wanatajwa kuwa miongoni mwa Mabondia waliotawala miaka [--] iliyopita ya maisha yao kabla ya kustaafu. Mchezo wa Rumble in the Jungle ni miongoni mwa pambano la Ndondi maarufu duniani lililowakutanisha ngumi mashuhuri Mohammad Ali na George Foreman lililofanyika mjini Kinshasa nchini Zaire (sasa DR Congo) chini ya utawala wa Rais Mobutu Sese Seko. Mike Tyson (59)aliwahi kuwa Bingwa namba moja duniani wa uzani wa juu lakini licha ya kustaafu mchezo"
X Link 2026-02-17T17:41Z 1.8M followers, [----] engagements

"Bw. Mafuru tutakukumbuka kwa kujitolea kwako bidii na mchango wako katika Maendeleo ya Tanzania. Goodbye Lawrence 🕊 Sleep well.Till we meet again brother 🙏"
X Link 2024-11-09T14:03Z 1.7M followers, 52.5K engagements

"38' GOOOAL Bruno Fernandes anaiandikia Manchester United bao la pili akiandika bao lake la pili kwenye mchezo dhidi ya Leicester City katika dimba la Old Trafford. Man United 2-0 Leicester City #KitengeSports"
X Link 2024-11-10T14:45Z 1.7M followers, [----] engagements

"Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Padre Charles Kitima amesema Wananchi wanapaswa kuachiwa wachague nani kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa badala ya kuingiliwa na kuenguliwa kwa baadhi ya Wagombea wa Vyama vya Upinzani. #KitengeUpdates"
X Link 2024-11-10T15:53Z 1.7M followers, 33.8K engagements

"📝 : Klabu ya AS Roma imemfuta kazi mkufunzi Ivan Juric kufuatia msururu wa matokeo yasiyoridhisha kikiwemo kipigo cha 3-2 dhidi ya Bologna kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Italia siku ya Jumapili. Juric raia wa Croatia ameondoshwa kwenye hatamu ya uongozi wa klabu hiyo ikiwa ni chini ya miezi miwili tangu alipoteuliwa kuwa kocha mkuu kwa mkataba mpaka Juni [----] akichukua mikoba ya Daniele De Rossi. #KitengeSports"
X Link 2024-11-10T17:52Z 1.7M followers, 21.1K engagements

"60' GOOOAL Gabriel Martinelli anaiandikia Arsenal bao la uongozi dhidi ya Chelsea katika dimba la Stamford Bridge kwenye Derby ya London. Chelsea 0-1 Arsenal #KitengeSports"
X Link 2024-11-10T17:55Z 1.7M followers, [----] engagements

"Ruben Amorim amemaliza kwa kishindo muda wake kama kocha wa Sporting Lisbon kabla ya kutimkia Manchester United baada ya kuiongoza klabu hiyo kutoka nyuma 2-0 na kushinda 4-2 dhidi ya Braga kwenye mechi ya mwisho klabuni hapo. Amorim (39) raia wa Ureno ambaye tayari ametangazwa kama kocha mkuu mpya wa Man United anatarajiwa kuanza kazi hiyo kuanzia kesho Novemba [--] [----] ingawa ripoti zinaeleza kwamba hatoanza kazi mpaka apate vibali vya kazi (work permit) FT: Braga 2-4 Sporting Lisbon ⚽ 20' Horta ⚽ 45' Horta ⚽ 57' Morita ⚽ 81' Hjulmand ⚽ 89' Harder ⚽ 90+4' Harder #KitengeSports"
X Link 2024-11-10T21:40Z 1.7M followers, 37K engagements

"Sheikh Salum Nayabagabo amechaguliwa kuwa Mkuu wa Jumuiya ya Kiislamu ya nchini Burundi baada ya kuongoza ofisi ya mkoa wa Comibu mkoani Muyinga kwa zaidi ya miaka [--]. Sheikh Salum Nayabagabo anamrithi Sheikh Sadiki Kajandi Abdallah ambaye aliandika barua ya kujiuzulu mnamo [----] kufuatia ugomvi ndani ya Comibu. Sheikh Salum Nayabagabo baada ya kuchaguliwa amewaomba Waislamu kujiendeleza na kuimarisha usalama wa nchi. #KitengeUpdates"
X Link 2024-11-11T10:32Z 1.7M followers, 13.8K engagements

"Kijana Zakaria Ahmed Kayanda akiwa Seattle Marekani yeye anashangazwa sana na Watangazaji wa Tanzania kuchanganya Kiswahili na Kiingereza katika kutangaza"
X Link 2024-11-11T11:14Z 1.7M followers, 79.4K engagements

"Klabu ya Amasipiri FC ya mjini Bujumbura inakwenda kupigwa faini ya Laki tano Faranga za Burundi baada ya kushindwa kufika Uwanjani kucheza mchezo wa wiki ya kumi wa Ligi Kuu Burundi dhidi ya Aigle Noir ya mkoani Makamba. Amasipiri FC ambayo imeanza kwa kusua sua Ligi Kuu nchini Burundi haikuweka wazi sababu za kushindwa kusafiri kuwafuata The Eagle mchezo ambao ungepigwa katika Uwanja wa NPPC. Hata hivyo kwa upande wa Kocha Mkuu wa timu ya Amasipiri FC Simon Gakinja ambaye aliwahi kuifundisha Deira FC amebainisha kuwa moja wapo ya sababu za kushindwa kusafiri ni ukosefu wa mafuta. Kwa upande"
X Link 2024-11-11T16:42Z 1.7M followers, [----] engagements

"MGOGORO WA ZANZIBAR WACHUKUA SURA MPYA"
X Link 2024-11-12T09:39Z 1.7M followers, 23.5K engagements

"Video inayotrend mitandaoni ikionesha mtu analazimishwa kwa nguvu kupakiwa kwenye gari lakini mwenyewe akipiga kelele kuwa anaenda kuawa huku akigoma kupanda kwa gari hiyo. #KitengeUpdates"
X Link 2024-11-12T19:16Z 1.7M followers, 181.4K engagements

"Jeshi nchini Rwanda limethibitisha kumkamata Askari Jeshi mwenye cheo cha Sajenti baada ya kuripotiwa kuwaua kwa kuwafyatulia risasi maeneo ya Nyamasheke. Katika tangazo fupi ambalo limetolewa na Jeshi la Rwanda lisasema kuwa Askari Jeshi huyo mwenye umri wa miaka [--] alikuwa ni Mwanajeshi katika Jeshi la Rwanda. Gervais MINANI alikamatwa baada ya kutenda uovu huouchunguzi ukiwa umeanza kufanyika Jeshi lilisema. Baadhi ya taarifa zinasema kuwa mauaji hayo yalifanyikia katika ukumbi wa starehe baada ya kutokea kwa maelewano mabaya na ambao walikuwepo maeneo hayo. Tukio hilo linakuja baada ya"
X Link 2024-11-13T19:50Z 1.7M followers, 25.6K engagements

"Mtuhumiwa Mkuu katika kesi ya wizi wa takribani Shilingi Bilioni [---] za Benki ya Equity nchini Kenya Bw.John Karima Wainaina amekamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyata akitokea China. Wainaina alikimbilia China mnamo mwezi Julai wakati Uchunguzi wa kesi hiyo ukiendelea. Kwa kufuatilia simu na mitandao ya kijami kitengo cha Uchunguzi wa ulaghai wa Benki pamoja na huduma ya intelijensia walifanikiwa kumhusisha Mtuhumiwa na kundi lililomuajiri Meneja wa Benki David Machiri na kufanya miamala ya ulaghai zaidi ya [--]. Wahusika walifanikiwa kutoa pesa kupitia mfumo wa ulipaji"
X Link 2024-11-14T07:17Z 1.7M followers, 45.8K engagements

"Balozi Mteule wa Jamhuri ya Korea Nchini Tanzania Mhe. Balozi Eunju Ahn Novemba [--] [----] amefanya ziara ya kutembelea Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha na Kituo cha Polisi Utalii na Diplomasia lengo likiwa ni kuimarisha mahusiano baina yao na Jeshi la Polisi. Balozi Eunju ameeleza Serikali ya Korea imefungua milango kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa Askari Polisi ili kuwajengea uwezo ambapo ofisi ya Ubalozi huo itatoa ushirikiano katika mafunzo kwa Askari kwenda Korea kujifunza namna nchi hiyo inavyofanya kazi katika masuala ya Ulinzi na Usalama. Katika ziara hiyo Mheshimiwa Balozi Eunju"
X Link 2024-11-14T18:25Z 1.7M followers, [----] engagements

"Mwanamuziki Mkongwe Kikumbi Mwanza Mpango King Kikii amefariki dunia. Mwanamuziki huyo ambaye ameugua kwa muda mrefu amefariki usiku wa kuamkia leo katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili ambako alikuwa amelazwa. Atakumbukwa King Kikii kwa wimbo wake uliotamba mno wa Kitambaa Cheupe. Pumzika kwa amani Mzee wa Kitambaa Cheupe King Kikii.🙏"
X Link 2024-11-15T03:54Z 1.7M followers, 99.2K engagements

"Patrice Motsepe wa Afrika Kusini anatarajia kurejea kwa muhula wa pili kama Rais wa Shirikisho la soka la Afrika (CAF) baada ya kuwa Mgombea pekee katika nafasi hiyo. Motsepe alichukua mikoba ya Ahmad Ahmad wa Madagascar Machi [----] na sasa anatazamiwa kuendelea kuongoza bodi inayosimamia soka barani Afrika baada ya kutokuwa na mpinzani. Kando na kura ya Urais wa CAF uchaguzi pia utaamua Wajumbe wapya wa Kamati ya Utendaji ya CAF na Wawakilishi wa Afrika kwenye Baraza la FIFA. Amaju Pinnick wa Nigeria na Fouzi Lekjaa wa Morocco ni wanachama wa Baraza la FIFA na wanatarajia kutetea viti vyao."
X Link 2024-11-15T05:52Z 1.7M followers, 18.5K engagements

"Uganda Cranes ndio timu ya kwanza katika Ukanda wa CECAFA kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika la TotalEnergies (AFCON) [----]. Kikosi cha Kocha Paul Put kilinufaika na majirani Sudan Kusini ambao waliwashinda wachezaji [--] Congo Brazzaville 3-2 katika mechi ya Kundi K iliyochezwa mapema huko Juba Alhamisi. Ushindi wa Sudan Kusini unamaanisha Uganda na Afrika Kusini ambazo zitamenyana leo zote zimefuzu kabla ya kucheza mechi zao mbili zilizosalia. Uganda wanaongoza Kundi K wakiwa na pointi [--] huku Afrika Kusini wakiwa nafasi ya pili wakiwa na pointi [--]. Wawili hao watafuzu moja kwa moja kwa"
X Link 2024-11-15T08:27Z 1.7M followers, 10.3K engagements

"Uongozi wa klabu ya Yanga Sc umethibitisha kuvunja mkataba na kocha wa kikosi cha kwanza Miguel Angel Gamondi raia wa Argentina pamoja na kocha msaidizi Moussa Ndaw. Taarifa ya leo Novemba [--] [----] iliyotolewa na klabu hiyo imebainisha kuwa klabu hiyo tayari imeanza mchakato wa haraka wa kutafuta Makocha wapya wa kikosi hicho na unatarajiwa kukamilika hivi punde. Uongozi wa Young Africans Sports Club unapenda kuwashukuru Makocha hao kwa mchango wao ndani ya Klabu yetu na unawatakia kila la kheri katika majukumu yao mapya. imesema sehemu ya taarifa hiyo. #KitengeSports"
X Link 2024-11-15T09:22Z 1.7M followers, 69.4K engagements

"Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeitoza klabu ya Azam Fc faini ya Tsh milioni tatu kwa kosa la kuzuia wapigapicha wa mdhamini mwenye haki za matangazo ya runinga Azam TV kurekodi picha jongeo wakati timu hiyo ikiingia katika uwanja wa Azam Complex kuelekea mchezo wao dhidi ya Young Africans Sc uliomalizika kwa Azam Fc kuibuka na ushindi wa 1-0. #KitengeSports"
X Link 2024-11-15T12:37Z 1.7M followers, 92.4K engagements

"BREAKING: Klabu ya Yanga imemtambulisha Sead Ramovic raia wa Ujerumani kuwa kocha wao Mpya akirithi mikoba ya Gamondi. Sead Ramovic alikuwa kocha mkuu wa timu ya Ts galaxy ya Afrika ya kusini. #KitengeSports"
X Link 2024-11-15T14:25Z 1.7M followers, 18.9K engagements

"KOCHA mpya wa Yanga Sc Sead Ramovic ambaye ni muumini wa mfumo wa 4-2-3-1 akiwa na TS Galaxy ya Afrika Kusini kwenye mechi [--] za ligi hajashinda mechi hata moja sare [--] na vipigo vinne. Mjerumani huyo mwenye umri wa miaka [--] ameiongoza TS Galaxy kuvuna alama [--] tu huku timu hiyo ambayo ipo mkiani mwa msimamo wa ligi ikifunga magoli [--] na kuruhusu [--]. #KitengeSports"
X Link 2024-11-15T14:55Z 1.7M followers, 107.3K engagements

"Kocha Mpya wa Yanga Sead Ramovic ukifanya Starehe kwake ukiwa mchezaji umekwisha✍🏼"
X Link 2024-11-15T18:04Z 1.7M followers, 75.8K engagements

"Kwa Marafiki na Jamaa wa Mpendwa Wetu Marehemu Kikumbi Mwanza Mpango Mwema ( King Kikii) ambao wangependa kujumuika pamoja kumsindikiza kwenye Safari yake ya Mwisho Msiba upo Nyumbani kwake Mtoni Kwa Aziz Ally wanatazamana na Kituo Cha Mwendokasi kama Unaenda Temeke. Mnakaribishwa wote kushiriki pamoja kutoa Faraja kwa Familia na Kumsindikiza kwenye Nyumba yake ya Milele. Bwana Alitoa na Katwaa. 😭"
X Link 2024-11-15T19:35Z 1.7M followers, [----] engagements

"Klabu ya Juventus ya Italia imetangaza kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba wa kiungo Paul Pogba kwa makubaliano ya pande zote kuanzia Novemba [--] [----] licha ya nyota huyo kupunguziwa adhabu. Klabu ya Juventus na Paul Pogba wanatangaza kuwa wameamua kwa makubaliano ya pande zote kusitisha mkataba wao wa ajira kuanzia tarehe [--] Novemba [----] imesema taarifa ya Kibibi Kizee hicho cha Turin. Pogba [--] ambaye mkataba wake na Juventus ulikuwa utamatike Juni [----] alifungiwa kujihusisha na soka kwa miaka minne baada ya kukutwa na hatia ya matumizi ya dawa za kusisimua misuli aina ya"
X Link 2024-11-15T20:15Z 1.7M followers, 28.2K engagements

"Timu ya taifa ya Zambia Chipolopolo imefuzu kwenda AFCON [----] baada ya kuwalaza Mabingwa watetezi Ivory Coast kwenye mchezo wa raundi ya [--] wa kufuzu michuano hiyo itakayofanyika Nchini Morocco. Bao pekee la Kennedy Musonda limewapeleka Chipolopolo kileleni mwa Kundi G wakifikisha pointi [--] baada ya mechi [--] huku Ivory Coast wakiporomoka mpaka nafasi ya pili wakiwa na pointi [--]. Sierra Leone wanakamata nafasi ya tatu wakiwa na pointi [--] huku Chad wakiburuza mkia wakiwa na pointi tatu. FT: Zambia 1-0 Ivory Coast ⚽ 43' Musonda #KitengeSports"
X Link 2024-11-15T20:31Z 1.7M followers, 45.8K engagements

"CRISTIANO Ronaldo amefunga bao lake la [---] kwenye maisha yake ya soka akiifungia Ureno mabao mawili kwenye ushindi wa 5-1 dhidi ya Poland kwenye mchezo wa UEFA Nations League. Katika mchezo mwingine Uhispania imeilaza Denmark 2-1 huku Croatia iliyokuwa pungufu ya mchezaji ikilala 1-0 dhidi ya Scotland wakati Uswisi wakitoshana nguvu na Serbia kwa sare ya 1-1. FT: Portugal 5-1 Poland ⚽ 59' Leak ⚽ 72' Ronaldo (P) ⚽ 80' Bruno ⚽ 83' Neto ⚽ 87' Ronaldo ⚽ 89' Marczuk FT: Denmark 1-2 Spain ⚽ 84' Isaksen ⚽ 15' Oyarzabal ⚽ 58' Perez FT: Switzerland 1-1 Serbia FT: Scotland 🏴 1-0 Croatia #KitengeSports"
X Link 2024-11-16T03:30Z 1.7M followers, 19.5K engagements

"Gwiji wa ngumi za kulipwa za uzito wa juu Duniani Mike Iron Tyson amepoteza pambano lake la raundi nane dhidi ya mtengeneza maudhui ya mtandao wa YouTube Jake Paul kwa pointi za majaji wote watatu Asubuhi hii nchini Marekani. Jaji namba moja Lawrence Cole wa Marekani ame-score pointi 73-79 jaji namba mbili David Lacobucci wa Marekani yeye ame-score pointi 72-80 na jaji namba tatu Jesse Reyes wa Marekani ame-score pointi 73-79. Hili ni pambano la saba kwa Mike Tyson kupoteza katika mapambano [--] ya ngumi za kulipwa aliyocheza kwa Jake Paul huu ni ushindi wake wa [--] katika mapambano 12"
X Link 2024-11-16T06:39Z 1.7M followers, 15.1K engagements

"Taarifa zilizotufikia zinasema Jengo la ghorofa limeporoka Kariakoo na Congo Jijini Dar es Salaam. Jitihada za kuokoa vitu na manusura wa ajali hiyo zinaendelea✍ #KitengeIpdates"
X Link 2024-11-16T07:07Z 1.7M followers, 81.9K engagements

"Hali ilivyo kariakoo muda huu✍"
X Link 2024-11-16T07:40Z 1.7M followers, 70.5K engagements

"TIMU ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itashuka dimbani leo Novemba [--] [----] kwenye mchezo wa kuwania kufuzu kombe la Mataifa Afrika AFCON [----] dhidi ya Ethiopia katika uwanja wa Taifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (Martyrs de la Pentecote) ikihitaji kufufua matumaini yake ya kukata tiketi ya AFCON [----]. Wenyeji Ethiopia ambao wamechagua uwanja wa Martyrs de la Pentecote kuwa uwanja wao wa nyumbani wapo mkiani mwa msimamo wa kundi H pointi [--] baada ya mechi nne huku Stars ambayo inahitaji kusahau vipigo viwili mfululizo dhidi ya DR Congo kwenye mechi mbili zilizopita ikishika nafasi ya"
X Link 2024-11-16T08:42Z 1.7M followers, 11.8K engagements

"Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila Yuko tayari Kariakoo kwenye eneo lilipoporomoka Ghorofa. #KitengeUpdates"
X Link 2024-11-16T08:54Z 1.7M followers, 65.6K engagements

"Hali ilivyo Kariakoo muda huu baada ya kutokea ajali ya kuporomoka kwa Ghorofa. #KitengeUpdates"
X Link 2024-11-16T09:28Z 1.7M followers, 41.4K engagements

"Vifaa mbali mbali kwa ajili ya Uokozi vimeendelea kuwasili Kariakoo ili kuokoa watu waliopo kwenye vifusi kufuatia ajali ya kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo. #KitengeUpdates"
X Link 2024-11-16T09:55Z 1.8M followers, [--] engagements

"15' GOOOAL Simon Happygod Msuva anaiandikia Taifa Stars bao la uongozi dhidi ya Ethiopia. Ethiopia 0-1 Tanzania #KitengeSports"
X Link 2024-11-16T16:16Z 1.7M followers, [----] engagements

"31' GOOAL Faisal Salum 'Feitoto' anaiandikia Stars bao la pili dhidi ya Ethiopia katika uwanja wa Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Ethiopia 0-2 Tanzania #KitengeSports"
X Link 2024-11-16T16:32Z 1.7M followers, [----] engagements

"Taifa Stars ipo mbele 2-0 mpaka mapumziko dhidi ya Ethiopia kwenye mchezo wa Kundi H kuwania kufuzu kombe la Mataifa Afrika AFCON [----]. HT: Ethiopia 0-2 Tanzania ⚽ 15' Msuva ⚽ 31' Feitoto #KitengeSports"
X Link 2024-11-16T16:55Z 1.7M followers, [----] engagements

"Timu ya taifa ya Tanzania imefuta uteja mbele ya Ethiopia baada ya kushinda kwa mara ya kwanza kihistoria dhidi ya Wahabeshi hao na kuweka hai matumaini ya kufuzu AFCON [----]. Kwa ushindi huo wa mabao 2-0 Stars imekwea mpaka nafasi ya pili ikifikisha pointi [--] baada ya mechi [--] huku Ethiopia ikiendelea kusalia mkiani pointi [--] baada ya mechi [--]. FT: Ethiopia 0-2 Tanzania ⚽ 15' Msuva ⚽ 31' Feitoto MSIMAMO Kundi H DR Congo Pts [--] Tanzania Pts [--] Guinea Pts [--] Ethiopia [--] Baadaye: Guinea vs DR Congo #KitengeSports"
X Link 2024-11-16T18:16Z 1.7M followers, 11.1K engagements

"Serhou Guirassy amefunga bao lake la [--] kwenye michuano ya kufuzu AFCON [----] akiifungia Guinea bao la ushindi jioni kabisa dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kufifisha matumaini ya Tanzania kufuzu AFCON [----]. Guinea wamefikisha pointi [--] na wamekwea mpaka nafasi ya pili huku Stars yenye pointi [--] wakiporomoka mpaka nafasi ya tatu. Mchezo wa mwisho utakaozikutanisha Tanzania na Guinea utaamua timu itakayokata tiketi ya AFCON [----] ambapo Stars ikiwa nyumbani utalazimika kushinda ili kufuzu. FT: Guinea 1-0 DR Congo ⚽ 90+2' Guirassy #KitengeSports"
X Link 2024-11-16T21:21Z 1.7M followers, 22.1K engagements

"Bondia wa Tanzania Hassan Mwakinyo amefanikiwa kuutetea kwa mara ya pili mfululizo ubingwa wake wa WBO Africa Middleweight kufuatia ushindi wa TKO raundi ya tisa (9) dhidi ya Daniel Lartey wa Ghana katika pambano lilochezwa usiku wa kuamkia Jumapili katika ukumbi wa Were House Masaki Dar es Salaam. Kufuatia ushindi huo Mwakinyo amemwaga machozi kutokana na kile alichosema ni Chuki za wazi kwa watu waliotakiwa kumsaidia kwenye mchezo wa Ngumi. Hata hivyo Mwakinyo amekabidhiwa Shilingi Milioni [--] ikiwa ni hamasa ya KO ya Mama. #KitengeSports"
X Link 2024-11-17T04:04Z 1.7M followers, 46.6K engagements

"Kamanda Mstaafu wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova akieleza hali ilivyo Kariakoo✍"
X Link 2024-11-17T08:23Z 1.7M followers, 46.7K engagements

"Mtu mwingine amejirekodi video akiwa chini ya kifusi akiomba msaada ya kuokolewa✍ #PrayForKariakoo"
X Link 2024-11-17T12:10Z 1.8M followers, [--] engagements

"MATOKEO: UEFA NATIONS LEAGUE Spain 3-2 Switzerland Croatia 1-1 Portugal Poland 1-2 Scotland 🏴 Serbia 0-0 Denmark Romania 4-1 Cyprus Kosovo 1-0 Lithuania Bulgaria 1-1 Belarus Luxembourg 2-2 Northern Ireland Liechtenstein 1-3 San Marino TIMU ZILIZOFUZU ROBO FAINALI Group 1: Portugal & Croatia Group 2: France & Italy Group 3: Germany & Netherlands Group 4: Spain & Denmark #KitengeSports"
X Link 2024-11-19T03:42Z 1.7M followers, [----] engagements

"TOTO AFYA YADODA"
X Link 2024-11-26T07:33Z 1.7M followers, [----] engagements

"Shangwe la Wazee wa Minyama na @Official_JUX wakicheza Ololufe Mi ya @Official_JUX aliomshirikisha @diamondplatnumz"
X Link 2024-11-26T09:07Z 1.7M followers, 24.8K engagements

"63' GOOOAL Adama Coulibaly anaitanguliza Al Hilal Omdurman dhidi ya Wananchi Young Africans SC katika dimba la Benjamin Mkapa. YANGA SC 0-1 AL HILAL #KitengeSports"
X Link 2024-11-26T14:22Z 1.7M followers, 11.3K engagements

"Droo ya raundi ya tatu ya kombe la FA England imetoka huku Mabingwa watetezi Manchester United wakipewa mfupa mgumu Arsenal huku Manchester City ikipewa vibonde Salford City inayoshiriki League Two England (ligi daraja la nne Nchini England). Liverpool itakuwa wenyeji wa Accrington Stanley katika dimba la Anfield huku Chelsea wakiwakaribisha Morecambe wakati Tottenham ikiwafuata Tamworth inayoshiriki ligi daraja la [--] England. DROO FA CUP (Mechi za raundi ya tatu zitachezwa mwisho wa wiki ya Januari [--] na [--] 2025) Arsenal v Manchester United Manchester City v Salford City Liverpool v"
X Link 2024-12-02T20:13Z 1.7M followers, 15.7K engagements

"DP WORLD YAPAISHA MAPATO TRA YAKUSANYA TRIL [----] MIEZI 5"
X Link 2024-12-04T06:56Z 1.7M followers, 16.9K engagements

"BEL YA NYAMA YAWASHITUA WAZEE WA MINYAMA"
X Link 2024-12-05T03:36Z 1.7M followers, [---] engagements

"Wazee wa Minyama leo uso kwa uso na Mwana historia mahiri Mohamed Said alipotutembelea Leo Studio. @Gerald_Hando @musakipanya @Zembwelabeberu"
X Link 2024-12-16T06:08Z 1.7M followers, [----] engagements

"Mwamba Ghalib Said Mohamed GSM 🤝"
X Link 2024-12-17T17:06Z 1.7M followers, 61.1K engagements

"42' GOOOAL Ibrahim Hamad 'Bacca' anaiandikia Yanga Sc bao la pili dhidi ya Wajelajela Tanzania Prisons katika dimba la KMC Complex. Yanga Sc 2-0 TZ Prisons #KitengeSports"
X Link 2024-12-22T13:43Z 1.7M followers, [----] engagements

"Gusa achia twende kwao imepigwa kwa kiingereza aiseee😆 Mbona kama wana Yanga wana confidence sana 😄 Yanga Sc 3-1 TP Mazembe #KitengeSports"
X Link 2025-01-04T22:05Z 1.7M followers, 63.7K engagements

"Wenyeji Liverpool wamebanwa nyumbani dhidi ya Mashetani Wekundu Manchester United katika dimba la Anfield FT: Liverpool 2-2 Man United ⚽ 59' Gakpo ⚽ 70' Salah (P) ⚽ 52' Martinez ⚽ 80' Amad FT: Fulham 2-2 Ipswich #KitengeSports"
X Link 2025-01-05T18:48Z 1.7M followers, [----] engagements

"Minyama inalika hapa Doha Qatar"
X Link 2025-01-12T12:21Z 1.8M followers, 31.6K engagements

"Chris Wood amefunga bao lake la [--] la msimu akiitanguliza Nottingham Forest dhidi ya Liverpool. 15' Forest 1-0 Liverpool ⚽ 8' Wood #KitengeSports"
X Link 2025-01-14T20:27Z 1.8M followers, 21.9K engagements

"68' Antoine Semenyo ameitanguliza Bournemouth dhidi ya Chelsea katika dimba la Stamford Bridge. Chelsea 1-2 Bournemouth ⚽ [--] Palmer ⚽ 50' Kluivert (P) ⚽ 68' Semenyo #KitengeSports"
X Link 2025-01-14T21:05Z 1.8M followers, 10.5K engagements

"Manchester City imeitolea uvivu Ipswich Town kwa kuishindilia jumla ya magoli 6-0 katika dimba la Portman Road. FT: Ipswich 0-6 Man City ⚽ 27' Foden ⚽ 30' Kovai ⚽ 42' Foden ⚽ 49' Doku ⚽ 57' Haaland ⚽ 69' McAtee #KitengeSports"
X Link 2025-01-19T18:49Z 1.8M followers, 14.4K engagements

"@jokateM Naam"
X Link 2025-01-20T06:28Z 1.8M followers, 20.6K engagements

"@JonMrema Duh"
X Link 2025-01-22T21:01Z 1.8M followers, 27.1K engagements

"Manchester United imetinga hatua ya [--] ya michuano ya Europa League kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi ya FCSB Arena Nationala mjini Bucharest Romania ikiungana na Lazio Athletic Bilbao Tottenham Eintracht Frankfurt Lyon Olympiacos Piraeus na Rangers kwenye hatua hiyo. FCSB"
X Link 2025-01-31T02:32Z 1.8M followers, 17.5K engagements

"@bajabiri Aiseee"
X Link 2025-02-09T08:25Z 1.8M followers, [---] engagements

"Safarini Makka na Madina kwa ajili ya ibada ya Umrah"
X Link 2025-03-18T21:37Z 1.8M followers, 67.5K engagements

"Al Masjid Nabawi Madina"
X Link 2025-03-19T12:02Z 1.8M followers, 27.4K engagements

"Medina Saudi Arabia"
X Link 2025-03-19T21:46Z 1.8M followers, 10.3K engagements

": UEFA Nations League Croatia 2-0 France ⚽ 26' Budimir ⚽ 45+1' Perisic Denmark 0-0 Portugal Italy 1-0 Germany ⚽ 09' Tonali Netherlands 1-1 Spain ⚽ 28' Gakpo ⚽ 09' Williams #KitengeSports"
X Link 2025-03-20T20:52Z 1.8M followers, 10.3K engagements

": UEFA Nations League Croatia 2-0 France ⚽ 26' Budimir ⚽ 45+1' Perisic FT: Denmark 1-0 Portugal ⚽ 78' Hojlund FT: Italy 1-2 Germany ⚽ 09' Tonali ⚽ 49' Kleindienst ⚽ 76' Goretzka Netherlands 2-2 Spain ⚽ 28' Gakpo ⚽ 46' Reijnders ⚽ 09' Williams ⚽ 90+3' Merino #KitengeSports"
X Link 2025-03-21T00:44Z 1.8M followers, [--] engagements

"Glad for the Allah to see another year in full health. God is good. Happy birthday to me🎂"
X Link 2025-03-22T21:19Z 1.8M followers, 30.8K engagements

"Ujerumani Ufaransa Ureno na Uhispania zimetinga nusu fainali ya UEFA Nations League. FT: France 2-0 Croatia (Agg. 2-2) (P 5-4) ⚽ 52' Olise ⚽ 80' Dembele FT: Germany 3-3 Italy (agg. 5-4) ⚽30' Kimmich ⚽ 36' Musiala ⚽ 45' Kleindienst ⚽ 49" Kean ⚽ 69' Kean ⚽ 90+5' Raspadori FT: Portugal 5-2 Denmark (Agg. 5-3) ⚽ 38' Andersen (og) ⚽ 72' Ronaldo ⚽ 86' Trincao ⚽ 91' Trincao ⚽ 115' Ramos ⚽ 56' Kristensen ⚽ 86' Eriksen FT: Spain 3-3 Netherlands (Agg. 5-5) (P 5-4) ⚽ 06' Oyarzabal (P) ⚽ 67' Oyarzabal ⚽ 103' Yamal ⚽ 54' Depay ⚽ 79' Maatsen ⚽ 109' Simons NUSU FAINALI Germany vs Portugal Spain vs France"
X Link 2025-03-24T02:42Z 1.8M followers, 10.7K engagements

"Paris to Amsterdam Holland✈✈✈"
X Link 2025-05-10T15:30Z 1.8M followers, 10.9K engagements

"@mzeewauvinza @Heineken Hatariii"
X Link 2025-05-30T18:43Z 1.8M followers, [---] engagements

"NO REFORMS NO ELECTION INAVYOTIKISA MITANDAONI"
X Link 2025-06-09T07:56Z 1.8M followers, 26.1K engagements

"Wakati Ligi Kuu bara msimu wa 2024/25 ikielekea ukingoni huku timu zote zikisaliwa na raundi moja isipokuwa Simba na Yanga waliosaliwa na mechi mbili kila mmoja huu hapa msimamo wa ufungaji bora. Jean Ahoua: [--] Lionel Ateba: [--] Clement Mzize: [--] Prince Dube: [--] Jonathan Sowah: [--] Steven Mukwala: [--] Pacm Zouzoua: [--] Gibril Sillah: [--]. #KitengeSports"
X Link 2025-06-19T14:06Z 1.8M followers, [----] engagements

"Mzee wa Minyama Times Square New York"
X Link 2025-07-03T19:21Z 1.8M followers, [----] engagements

"Easy Sunday.Dubai"
X Link 2025-07-06T14:43Z 1.8M followers, [----] engagements

"Twende twende Kaka @AtikiAbdulkarim Kata Wese Okoa Maisha. Tukutane NBC Dodoma Marathon"
X Link 2025-07-17T14:52Z 1.8M followers, [----] engagements

"Safarini Barcelona Spain Mchana huu. Wacha tukakamilishe dili la Marcus Rashford kwa miamba Barcelona"
X Link 2025-07-21T12:05Z 1.8M followers, 16K engagements

"Touchdown Barcelona Spain"
X Link 2025-07-22T05:39Z 1.8M followers, [----] engagements

"Munich to Helsinki Finland na wakala wa Marcus Rashford. Deal imekamilika sasa ni misele"
X Link 2025-07-25T09:27Z 1.8M followers, [----] engagements

"Helsinki Finland to Vienna Austria✈✈✈"
X Link 2025-07-26T13:36Z 1.8M followers, [----] engagements

"London to Helsinki Finland ✈✈✈"
X Link 2025-08-24T17:19Z 1.8M followers, [----] engagements

"Kylian Mbapp amefunga magoli mawili huku Vinicius Junior akifunga moja na kusaidia 'assist' lingine wakati Real Madrid ikiilaza Real Oviedo 3-0 katika dimba la Nuevo Carlos Tartiere FT: Real Oviedo 0-3 Real Madrid ⚽ 37' Mbapp ( Arda Guler) ⚽ 83' Mbapp ( (Vinicius Jr) ⚽ 90+3' Vinicius Jr ( Brahim Diaz) #kitengeSports"
X Link 2025-08-24T22:05Z 1.8M followers, [----] engagements

"Bao la dakika za jioooni kutoka kwa kinda wa miaka [--] Rio Ngumoha limeipatia Liverpool ushindi wa 3-2 dhidi ya wenyeji Newcastle United katika dimba la St James' Park. FT: Newcastle 2-3 Liverpool ⚽ 57' Guimaraes 🟥 45+3' Gordon ⚽ 88' Osula ⚽ [--] Gravenberch ⚽ [--] Ekitike ⚽ 90+10' Ngumoha #KitengeSports"
X Link 2025-08-25T21:25Z 1.8M followers, [----] engagements

"Hatimaye Mashetani Wekundu Manchester United wamepata ushindi wa kwanza wa msimu baada ya kuilaza Burnley 3-2 kwa taabu sana katika dimba la Old Trafford. FT: Man United 3-2 Burnley ⚽ [--] Cullen ⚽ [--] Mbeumo ⚽ 90+7 Bruno ⚽ [--] Foster ⚽ [--] Anthony FT: Chelsea 2-0 Fulham FT: Wolves 2-3 Everton FT: Sunderland 2-1 Brentford FT: Tottenham 0-1 Bournemouth #KitengeSports"
X Link 2025-08-30T16:39Z 1.8M followers, [----] engagements

"70 Pacome Zouzoua anaiandikia Yanga Sc bao la uongozi dhidi ya Williete Sc ya Angola katika dimba la Benjamin Mkapa. Yanga Sc 1-0 Williete Sc (Agg. 4-0) ⚽ [--] Pacome #KitengeSports"
X Link 2025-09-27T15:42Z 1.8M followers, [----] engagements

"Dubai na Balozi wa Heshima Brazil-Zanzibar Abdulswammad Abdulrahim @Abdulsamad_tz 🤝 ✈✈"
X Link 2025-10-13T12:43Z 1.8M followers, 10.5K engagements

"Chelsea angalau mmekata kilimilimi cha Manchester City Shukrani kwa bao la Ivanovic"
X Link 2014-02-03T22:24Z 1.7M followers, [--] engagements

"#GabonMpakaKombeLADunia tuwaunge mkono Serengeti Boys. Tuwachangie kwa hali na mali wakapigane @jamalmalinzi"
X Link 2017-03-18T15:19Z 1.7M followers, [--] engagements

"Just posted a photo https://www.instagram.com/p/BSv-YzhB-PT/ https://www.instagram.com/p/BSv-YzhB-PT/"
X Link 2017-04-11T15:10Z 1.7M followers, [--] engagements

"LIVE: Serengeti Boys vs Niger @ SuperSport Football https://www.instagram.com/p/BUXM2YkDNFH/ https://www.instagram.com/p/BUXM2YkDNFH/"
X Link 2017-05-21T17:19Z 1.7M followers, [--] engagements

"Nini utabiri wako kwa Manchester City Unaitabiria nini msimu unaoanza @ Manchester Eithad Stadium https://www.instagram.com/p/BXYJlnUDHvk/ https://www.instagram.com/p/BXYJlnUDHvk/"
X Link 2017-08-04T15:44Z 1.7M followers, [--] engagements

"Nyumbani kwa Matajiri Manchester City. Eithad Stadium @ Manchester Eithad Stadium https://www.instagram.com/p/BXYKnq2jFFq/ https://www.instagram.com/p/BXYKnq2jFFq/"
X Link 2017-08-04T15:53Z 1.7M followers, [--] engagements

"Pale unahojiwa.Maana tumezoea kuhoji. @ Arsenal Football Club. Emirates Stadium. Club Level. https://www.instagram.com/p/BXaZ1Jjjhru/ https://www.instagram.com/p/BXaZ1Jjjhru/"
X Link 2017-08-05T12:44Z 1.7M followers, [--] engagements

"Ahsante Marcus Rashford 1-1 Stoke vs Man United.Ngoma inaendelea"
X Link 2017-09-09T17:20Z 1.7M followers, [---] engagements

"Easy Sunday. @ Dubai United Arab Emirates https://www.instagram.com/p/BY20_fcDJj9/ https://www.instagram.com/p/BY20_fcDJj9/"
X Link 2017-09-10T10:11Z 1.7M followers, [--] engagements

"Week end Dubai @ Dubai United Arab Emirates https://www.instagram.com/p/BY23ZVQhsv4/ https://www.instagram.com/p/BY23ZVQhsv4/"
X Link 2017-09-10T10:32Z 1.7M followers, [--] engagements

"Just posted a photo @ Dubai United Arab Emirates https://www.instagram.com/p/BY23hDzBFs_/ https://www.instagram.com/p/BY23hDzBFs_/"
X Link 2017-09-10T10:33Z 1.7M followers, [--] engagements

"Dubai with adellatillya @ Dubai United Arab Emirates https://www.instagram.com/p/BY5frdcjLSH/ https://www.instagram.com/p/BY5frdcjLSH/"
X Link 2017-09-11T11:03Z 1.7M followers, [--] engagements

"Dubai @ Dubai United Arab Emirates https://www.instagram.com/p/BY5kNrnh7Y-/ https://www.instagram.com/p/BY5kNrnh7Y-/"
X Link 2017-09-11T11:42Z 1.7M followers, [--] engagements

"Leo ndio leo.Pep Guardiola atachomekea koti. @ Fumba Beach Lodge https://www.instagram.com/p/BchNnRPB2Pa/ https://www.instagram.com/p/BchNnRPB2Pa/"
X Link 2017-12-10T10:50Z 1.7M followers, [--] engagements

Limited data mode. Full metrics available with subscription: lunarcrush.com/pricing